Thursday, 18 May 2017

Bwana Mungu nashangaa kabisa (How Great Thou Art)

Bwana Mungu nashangaa kabisa,
Nikifikiri jinsi ulivyo,
Nyota, ngurumo, vitu vyote pia,
Viumbavyo kwa uwezo wako.

Chorus:
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie,
Jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikitembea pote duniani,
Ndege huimba nawasikia,
Milima hupendeza macho sana,
Upepo nao nafurahia.
Chorus

Nikikumbuka vile wewe Mungu,
Ulivyompeleka mwanao,
Afe azichukue dhambi zetu,
Kuyatambua ni vigumu mno.

Chorus

Yesu Mwokozi atakaporudi,
Kunichukua kwenda mbinguni,
Nitaimba sifa zako milele,

Wote wajue jinsi ulivyo.

No comments:

Post a Comment

Niwikite Magegania by Sammy Irungu

Tha ciaku itiri mihaka kuona umuthi turi oo muoyo Hinya wa gicoka giaku, niguo utukinyitie haha Ti itheru wi Ebenezer, niwe mutuhei hinya...