Thursday, 18 May 2017

Msalabani pa mwokozi (Down at the Cross)

Msalabani pa mwokozi, hapo niliomba upozi,
Akaniokoa mpenzi, Mwana wa Mungu.
Chorus:
Mwana wa Mungu, Mwokozi wangu,
Akaniokoa mpenzi, Mwana wa Mungu.

Chini ya mti msumbufu, niliomba utakatifu,
Alinikomboa kwa damu, Mwana wa Mungu.
Chorus
Aliniokoa dhambini, ikawa kunikaa ndani,
Aliponifia mtini, Mwana wa Mungu.
Chorus
Damu ya Yesu ya thamani, huniokoa makosani,
Huniendesha wokovuni, Mwana wa Mungu.
Chorus                                                   
Hicho kijito cha gharama, leo jivike kwa kuzama,
Kwake uuone uzima, Mwana wa Mungu.



No comments:

Post a Comment

Niwikite Magegania by Sammy Irungu

Tha ciaku itiri mihaka kuona umuthi turi oo muoyo Hinya wa gicoka giaku, niguo utukinyitie haha Ti itheru wi Ebenezer, niwe mutuhei hinya...