Wamwendea Yesu
kwa kusafishwa,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake umemwagiwa?
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Chorus:
Kuoshwa, kwa damu,
Itutakasayo ya
kondoo,
Ziwe safi nguo nyeupe
mno,
Umeoshwa kwa damu ya
kondoo?
Wamwandama daima Mkombozi,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Yako kwa Msulubiwa makazi,
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Chorus
Atakapokuja Bwana-arusi,
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda mbinguni mavazi,
Yafuliwe kwa damu ya kondoo.
Chorus
Yatupwe yalipo na takataka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo,
Huoni kijito chatiririka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo?
No comments:
Post a Comment