Thursday, 18 May 2017

Kesha Ukiomba by Paul Mwai

Chorus:
Kesha ukiomba kesha ukiomba, 
Kesha ukiomba kesha ukiomba
Maana adui naye atafuta walio lala, 
Ili awaangamize roho yangu usilale

Majaribu na shida zimetusonga,
Shetani ajaribu kutuandama kila wakati
Mwenzangu tusimame imara kwa wokovu
Tukeshe tukiomba na yote tutashinda.
 Chorus
WaKristo tu wanyonge, wa mwili na wa roho,
Twamwomba Mungu wetu usiku na mchana
Atupe nguvu zake tushinde yule mwovu
Maana bila yeye sisi hatutaweza
 Chorus
Shambani Gethsemane Yesu aliomba
Baba kiondoe kikombe cha machozi
Maana sio mapenzi yangu yatimizwe
Bali mapenzi Yako Baba yatimizwe
Mungu kampa nguvu kashinda majaribu
Chorus 
Kilio ninacho mimi ni kwa wale wameokoka
Adui ameamua kamwe hatatuacha
Aleta majaribu usiku na mchana
Vijana nawaomba, wazee na watoto
Tusimame imara, na yote tutashinda


No comments:

Post a Comment

Niwikite Magegania by Sammy Irungu

Tha ciaku itiri mihaka kuona umuthi turi oo muoyo Hinya wa gicoka giaku, niguo utukinyitie haha Ti itheru wi Ebenezer, niwe mutuhei hinya...